Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2017

Serikali imeajiri walimu secondari na shule za msingi

Serikali inatarajia kuajiri Walimu 92 wa Shahada na 174 wa Stashahada wa masomo ya Fizikia, Hisabati, Kilimo na Biashara kwa Shule za Sekondari na Walimu 2,767 wa Cheti kwa Shule za Msingi. Waombaji kwa shule za Sekondari wawe waliohitimu mafunzo ya Ualimu mwaka 2016 au kabla, na wale wa Shule za Msingi wawe waliohitimu mafunzo yao mwaka 2014 au kabla.  Sifa za Waombaji: Walimu wa Sekondari: Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye somo moja la kufundishia au zaidi au Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo moja la kufundishia au zaidi pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali. Masomo ya kufundishia ni kati ya Fizikia, Hisabati, Kilimo au Biashara.Stashahada ya Ualimu katika masomo yaliyoainishwa kwenye kipengele Na. 2.1 (i) hapo juu.Cheti cha Kidato cha SitaCheti cha Kidato cha Nne Walimu wa Shule za Msingi: Astashahada ya Ualimu...

Nafasi za masomo chuo cha mwalimu nyerere memorial academy

Je una ndugu jama rafiki aliemaliza kidato cha sita na anahitaji kujiunga na chuo? basi habari njema ni hizi chuo cha mwalimu nyerere memorial academy kinatangaza udahili wa wanafunzi mwaka wa masomo 2017/2018 chuo kipo kigamboni dares salaam, pia kingine kipo zanzibar habar njema ni kwamba ukiomba tu! umesajiliwa ili mradi umekidhi vigezo vya kuingia chuo kikuu au waweza ingia mnma.ac.tz.kwa taarifa zaidi ,pia wiki hili yupo mwakilishi wa chuo iringa hapa anaweza kukusaidia kujisajili moja kwa moja. Kumbuka vyuo vyote hivi vipo kwenye fukwe za bahari maeneo mazur kujisomea na upepo mwanana.karibu sana Nisaidie kushare ili wahusika wengi zaidi ujumbe huu uwafikie. Asante!!