Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI 2017/2018


ENDELEA NAYO ;



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.
Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015.
Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.
Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni 96,018 sawa na asilimia 27.60 ya watahiniwa waliofanya mtihani Tanzania Bara.
Simbachawene alisema kutokana na mwongozo wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Mei 15, 2017 jumla ya wanafunzi 93,019 ndiyo wenye Sifa za kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa kuwa wamefaulu vigezo vyote vya msingi kama vilivyoaibishwa na Wizara ya elimu sayansi na teknolojia ambapo kati ya hao 92,998 ni wa shule na wanafunzi 21 ni wale waliosoma taasisi ya elimu ya watu wazima.
Aidha amewataka wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano kuwasili kwa wakati katika shule walizopangiwa July 17 mwaka huu na kwamba hakutakuwa na mabadiliko ya shule walizopangiwa.

"Na kama kuna mwanafunzi ambaye hataripoti kwenye shule aliyopangiwa kwa muda wa siku 14 nafasi yake itachukuliwa na mtu mwingine," alisema SimbachaweneBONYEZA HAPA KUTAZAMA

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nafasi za masomo chuo cha mwalimu nyerere memorial academy

Je una ndugu jama rafiki aliemaliza kidato cha sita na anahitaji kujiunga na chuo? basi habari njema ni hizi chuo cha mwalimu nyerere memorial academy kinatangaza udahili wa wanafunzi mwaka wa masomo 2017/2018 chuo kipo kigamboni dares salaam, pia kingine kipo zanzibar habar njema ni kwamba ukiomba tu! umesajiliwa ili mradi umekidhi vigezo vya kuingia chuo kikuu au waweza ingia mnma.ac.tz.kwa taarifa zaidi ,pia wiki hili yupo mwakilishi wa chuo iringa hapa anaweza kukusaidia kujisajili moja kwa moja. Kumbuka vyuo vyote hivi vipo kwenye fukwe za bahari maeneo mazur kujisomea na upepo mwanana.karibu sana Nisaidie kushare ili wahusika wengi zaidi ujumbe huu uwafikie. Asante!!

SECOND SELECTION KIDATO CHA TANO 2018/2019

Leo kumekuwa na habari za kuwekwa majina ya wanafunzi waliobahatika kujiunga Kidato Cha tano awamu ya pili ambapo wanafunzi hao wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangiwa mapema mwezi huu September kwa kuona majina tazama HAPA